16 Aprili 2025 - 16:58
Mufti wa Tanzania atangaza Dua ya Kuiombea Nchini na Wazee waliotangulia mbele ya Haki | Rais Samia Hassan na Rais Mwingi Kushiriki

Dua ya Kuiombea Taifa la Tanzania na kuwarehemu Wazee wetu waliotangulia mbele ya Haki itaongozwa na Mheshimiwa Mufti wa Tanzania.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Mufti wa Tanzania Shekh Abubakar bin Zuber ametangaza kuwepo kwa dua kubwa ya kuiombea nchi, Rais pamoja na wazee wetu waliotangulia mbele ya haki.

Mufti wa Tanzania atangaza Dua ya Kuiombea Nchini na Wazee waliotangulia mbele ya Haki | Rais Samia Hassan na Rais Mwingi Kushiriki

Dua hiyo inatarajiwa kufanyika kwa siku tatu mfululizo Kwa maana tarehe 8/9/10 mwezi wa tano 2025, katika Msikiti Mkuu wa Bakwata Kinondoni kwa siku mbili na kilele itakuwa tarehe kumi Jijini Dar.

Mufti wa Tanzania atangaza Dua ya Kuiombea Nchini na Wazee waliotangulia mbele ya Haki | Rais Samia Hassan na Rais Mwingi Kushiriki

Akitoa taarifa Kwa wanahabari Leo april 16 mchana huu alisema.... Nichukue nafasi hii kutoa taarifa ya kwamba tutakuwa na duwa kubwa ya kuiombea nchi Aman utulivu na kufungamana na tukio la kuwaombea wazee wetu waliotangulia mbele ya haki.  Pamoja na Mamuft wetu Shekh Hemedi bin Jumaa na Mufti Simba.

Mufti wa Tanzania atangaza Dua ya Kuiombea Nchini na Wazee waliotangulia mbele ya Haki | Rais Samia Hassan na Rais Mwingi Kushiriki

Mbali na hao pia wazee waliopigania Dini kwa hali na mali. Jambo hili ambalo lilianza rasmi Mwaka Jana ni muendelezo wa kila Mwaka chini ya Usimamizi wa Bi Mwantumu Mahiza na Alhaji Sued Twaibu ambao ndio waanzilishi wa jambo hili  

Katika mkutano huo wa Leo Mufti alikuwapo na Viongozi wakuu wa Bakwata pamoja na Viongozi wa Serikali kwa maana Wakuu wa Wilaya ya Ilala Kigamboni Temeke.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha